karibu

aisha

printers

classic

Tuesday, May 14, 2013

KASHFA MWANAUME ALIYELAZWA WODI YA WANAWAKE AMANA,MAPYA YAFICHUKA


MAAJABU zaidi yamebainika kuhusu kijana wa kiume, Karina Mohamed ‘Natalia’, 20, aliyelazwa wodi ya wanawake akidhaniwa ni mwanamke.
 
Karina Mohamed 'Natalia' akiwa katika hospitali ya Amana.
Karina, alilazwa wodi ya wanawake akidhaniwa ni mwanamke kwenye Hospitali ya Amana ambayo ina hadhi ya mkoa kitabibu, Ilala, Dar es Salaam, kabla ya kugundulika akiwa chumba cha maiti baada ya kufariki dunia.
Pamoja na habari hiyo ya Karina kuandikwa kwenye gazeti ndugu na hili la Risasi Jumamosi, toleo namba 1005 la Mei 4, mwaka huu, Uwazi limebaini maajabu yaliyofanya alazwe wodi ya wanawake kwa siku mbili bila kugundulika.

MAAJABU YA KWANZA; SURA
Timu ya gazeti hili imebaini kuwa sura ya Karina, haina tofauti yoyote na ya mwanamke.
Uwazi limepata ushahidi wa picha za Karina, enzi za uhai wake na kujiridhisha kwamba sura ya kijana huyo ilikuwa na sifa nyingi za kike kuliko za kiume.
 
Karina Mohamed 'Natalia' enzi za uhai wake.
MAAJABU YA PILI; UMBO